پایگاه اطلاع رسانی آیت الله ابراهیم امینی قدس سره

Mdhamini Wa Nyumba

Mdhamini Wa Nyumba

Kwa kawaida wanaume ni wafadhili wa familia. Hufanya bidii na hutumia mapato yao kwa wake zao na watoto wao. Wanaona huu ni wajibu wao na hawako tayari kuonesha kutokupendezwa na tatizo hili. Lakini pia wanaume wanategemea wake zao kutumia fedha zao kwa uangalifu na si kwa kufuja. Wanawake wanategemewa kuainisha mahitaji muhimu na kutumia fedha zao kwa uangalifu na si kwa kufuja. Wanawake wanategemewa kuainisha mahitaji muhimu na kutumia fedha kwa ajili ya vitu kama chakula, nguo, dawa, pango la nyumba, umeme, simu, moto wa gasi na maji.

Kuweka vitu kama hivyo kama mahitaji ya anasa katika orodha ya vitu muhimu hufikiriwa kuwa ni ufujaji. Wanaume hawapendi wake zao kutumia vibaya fedha zao katika kununua vitu visivyo vya muhimu au matumizi yanayo zidi kiasi.

Kama mwanaume anamuona mke wake mwaminifu katika kutunza fedha yake, kama anao uhakika, mke wake hatumii fedha kupita kiasi na kama anao uhakika kwamba fedha yake inayo patikana kwa shida haipotei bure, kwa hiyo, atafanya bidii zaidi na hatafuja fedha zake.

Kwa upande mwingine, kama mwanamke hutumia fedha za mume wake kununua nguo zake na mapambo yake au kama mke anatumia fedha katika kununua vitu visivyo muhimu na hadi waanze kukopa ili waweze kukidhi maisha, au kama familia, kama adui kafiri, hufuja utajiri wake basi mwanaume atakata tamaa. Hatapendelea kufanya kazi na kufadhili familia yake. Atadhani hakuna mantiki ya kufanya kazi na kusaidia watu ambao hawavutiwi na juhudi zake. Anaweza hata kukengeuka na kufuata njia yenye uovu. Tabia ambayo inaweza kuvunja misingi ya familia.

Bibi Mpendwa! Licha ya kwamba fedha za mume wako zimo katika utumiaji wako, usifikirie kwamba ni zako binafsi. Utajiri huo ni wa mumeo kisheria na wewe ni mdhamana. Kwa hiyo, kuchukua kitu chochote na kukifanya chako binafsi, kutoa kitu chochote, kutoa zawadi au kuuza kitu cha mumeo chochote, unahitaji ruhusa yake. Wewe unawajibika kwa mali ya mume wako na kwa vyovyote vile unatakiwa kuilinda. Ukikwepa wajibu wako, utakuwa na hoja ya kujibu Akhera.

“Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w) alisema: “Mwanamke ni mlinzi na mdhamini wa mali ya mume wake na katika hali hiyo anawajibika.”

“Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w) pia alisema: Mwanamke bora kuliko wote miongoni mwa wanawake wenu ni yule anayejipuliza manukato, hutayarisha chakula kitamu na hatavuka mpaka katika matumizi. Mwanamke wa aina hii ni mwakilishi na yu katika kundi la wafanyakazi wa Mwenyezi Mungu na mtu anayefanya kazi kwa ajili ya Mwenyezi Mungu kamwe hatapatwa na majuto au kushindwa.”

“Mwanamke alimuuliza Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w): “Ni zipi haki za mume kwa mke wake?” Mtume (s.a.w.w) alisema: “Mke lazima awe mtiifu kwa mumewe, asikiuke amri zake na asitoe kitu chochote bila ya ruhusa yake.”

Mtume wa Mwenyezi Mungu pia alisema(s.a.w.w): “Mwanamke bora kuzidi wote baina ya wanawake zenu ni yule anayetumia fedha kwa uangalifu.”