پایگاه اطلاع رسانی آیت الله ابراهیم امینی قدس سره

Mume Wako Akikasirika, Wewe Nyamaza

Mume Wako Akikasirika, Wewe Nyamaza

Mwanaume hukutana na watu wengi anapokuwa katika shughuli zake na hukabiliana na matatizo mengi. Anaporudi nyumbani, huwa amechoka na anapokutana na tukio dogo sana lisilofurahisha hukasirika na anaweza kuwa mkali kwa. familia yake.

Mwanamke mwenye busara atanyamaza wakati mume wake anajitapa kwa makelele yenye matusi. halafu mwanaume atanyamaza na kutulia na kujuta kwa matusi yake. Akiona kwamba hakuna jibu lolote kuhusu hasira yake, anaweza hata kuomba msamaha. Kwa msimamo huu, familia hurudi kwenye hali yake ya kawaida baada ya saa moja au mbili tu.

Hata hivyo, kama mwanamke wa nyumbani hakuelewa nafasi nyeti ya mume wake basi anaweza kupiga makelele, kuapa laana na kukasirika kwa ukali.

Kwa njia hii, mume na mke wanaweza kupigana na hatimaye kuchukua hatua ya kuachana. Familia nyingi huvunjika kwa sababu ya matukio madogo kama haya. Ipo hata mifano ambapo wanaume hukasirika sana hivyo kwamba hulipuka kama volcano na kufanya mauaji.

Mwanaume alimpiga risasi mke wake na mama wa kambo, na yeye mwenyewe akajipiga hadi kufa. Inafahamika kwamba wanandoa hao wana ugomvi mwingi na mabishano tangu mwanzo wa ndoa yao.

Usiku wa tukio hilo mume alirudi nyumbani kutoka kwenye shughuli zake ambapo wanandoa hao walianza tena ubishi mwingine.

Mume akampiga mke wake na mwanamke aliamua kwenda polisi. Haraka mwanaume alichukua bunduki, akamuua mke wake, mama yake wa kambo na halafu akajiua yeye mwenyewe kwa risasi.”

Si ingekuwa bora zaidi kama mwanamke angenyamaza wakati mume wake alikasirika? Kama mwanamke angevumilia, maisha ya watu watatu wangepotea? Wewe ungependelea vipi? Dakika chache za kimya au matokeo yote mabaya kwa kuendeleza ubishi na mume wako? Unadhani hata kwa dakika moja kwamba nafasi ya mwanaume inalindwa na kwa hiyo hana hatia. Si hivyo kabisa. Kama mambo yalivyo, anayo hatia.

Hakutakiwa kumaliza hasira yake kwa kumaliza familia yake. Kwenye sura ijayo, jambo hili litazungumziwa kwa kina zaidi lakini hapa tunasema kwamba mwanamke anatakiwa kuwa na busara na asijibu hasira ya mume wake hata kama mume yupo sawa au si sawa. Katika hali kama hii, mwanaume atashindwa kuthibiti hasira yake, kwa hiyo ni muhimu kwamba mke, anyamaze kimya ili aokoe familia yake.

Kwa kawaida wanawake hudhani kwamba kunyamaza kimya wanapokabiliana na hasira za waume zao, ni namna ya kudhalilishwa, na kwa hiyo wangepoteza hishima yao. Hata hivyo, hali hii ni kinyume chake. Mwanaume asiyeona jibu lolote anapomtukana mke wake, kwa hakika atajuta. Atamfikiria mke wake kuwa anampenda, ambaye licha ya uwezo wake wa kulipa kisasi alipendelea kusamehe. Mapenzi yake kwa mke wake yataongezeka mara nyingi. Ataomba msamaha na kwa hiyo mkewe atapata heshima zaidi.

Mtume (s.a.w.w) alisema: “Mwanamke yeyote ambaye huvumilia hasira mbaya ya mume wake Mwenyezi Mungu atampa thawabu zinazolingana na zile Alizompa Asiya binti Muzahim.”

Mtume (s.a.w.w) alisema: “Mwanamke aliyebora zaidi miongoni mwa wanawake zenu ni yule ambaye, akiona hasira ya mume wake humwambia; Nina jisalimisha kwako. Siwezi kulala hadi utakaporidhika na mimi.”

Mtume (s.a.w.w) alisema: “Usamehevu na uvumilivu ungeongeza heshima na hadhi ya wahusika. Uwe msamehevu ili Mwenyezi Mungu akuhifadhi.”