پایگاه اطلاع رسانی آیت الله ابراهیم امینی قدس سره

Usimwangalie Mtu Yeyote Isipokuwa Mumeo

Usimwangalie Mtu Yeyote Isipokuwa Mumeo

Mpendwa Bibi! Kabla hujaolewa inaewezekana ulikwisha chumbiwa na watu wengine. Posa za uchumba huu inawezekana zilitoka kwa watu matajiri, wasomi, wenye sura nzuri na kadhalika ambao ungependa wakuoe.

Matarajio ya aina hiyo yalikuwa ni jambo la kawaida kabla ya kuolewa. Lakini sasa umechagua mwenzi wako na kuwekeana mkataba wa dhati naye kuwa wapenzi katika maisha yenu yote, hivyo, sahau yaliyopita kabisa. Lazima uyaweke pembeni matamanio yako ya zamani na usahau ofa hizo za zamani. Usimfikirie mwamanume mwingine yeyote isipokuwa mumeo na utafute amani naye. Kama ukifanya vinginevyo, utajiweka katika hali ya mashaka.

Sasa basi, umekubali kuishi na mumeo, kwa nini wakati wote uendelee kuwatilia maanani wanaume wengine? Kwa nini umlinganishe mumeo na wanaume wengine? Unapata manufaa gani unapowatazama na kuwatilia maanani wanaume wengine isipokuwa kujiweka katika hali ya mateso yasiyo na mwisho na kusababisha upate maumivu makali ya akili?

Imam Ali (a.s) alisema: “Yeyote anayeyaacha macho yake huru, kila mara atapata maumivu ya neva na atanasa kwenye mtego wa wivu wakati wote.”

Kwa kuwatazama waume wengine na kuwatilia maanani na kuwalinganisha na mumeo, utamuona mwanaume ambaye hana dosari za mumeo. Unaweza kudhani kwamba labda mwamaume huyo amekamilika kwa sababu huzijui dosari za mwanaume huyo. Utafikiria kuwa ndoa yako ina mushkeli, na fikira hii inaweza ikawafikisheni mahali penye mwisho wenye hatari.

Mke wa mtu, umri wake miaka 18 ambaye alitoroka nyumbani kwake alikamatwa na polisi usiku wa jana. Akiwa kituo cha polisi mwanamke huyu alisema kwamba baada ya miaka mitatu ya ndoa, pole pole alihisi kwamba hampendi mume wake. Alisema: “Nilikuwa na tabia ya kulinganisha uso wa mume wangu na nyuso za wanaume wengine na nikajuta kwa nini niliolewa naye.”

Mpendwa Bibi! kama unataka ndoa ya kudumu daima milele, kama hutaki mateso ya kiakili, na kama unataka muendeshe maisha ya kawaida, basi acha kuwa mbinafsi na sahau hayo matarajio yako yasiyofaa. Usiwapongeze wanaume wengine. Usimfikirie mwanaume yeyote isipokuwa mumeo. Usiendekeze fikira hizi:

‘Afadhali ningeolewa na fulani’

‘Ningependa mume wangu aonekane kama . . . . . .’

‘Natamaani mume wangu angefanya kazi ya. . .. . . . . .’

‘Natamaani….. Natamaani……. Natamaani….’

Kwa nini ujifunge jela kwa kuendekeza mawazo hayo? Kwa nini utibue misingi ya ndoa yako? Kama lolote kati ya matakwa hayo yangefanikiwa kwa kweli, ungejuaje kwamba ungefanikiwa kuridhika zaidi? Unao uhakika kwamba wake za waume wajulikanao kama ‘hawana dosari; wanaridhishwa nao?

Mpendwa Bibi! Kama mumeo anashuku kwamba unaonesha kuvutiwa na wanamume wengine, atakata tamaa na kuacha kuvutiwa na wewe. Usitaniane na wanamume wengine au kufuatana nao. Wanamume ni wepesi kuhisi hivyo kwamba hawawezi hata kuvumilia wake zao kuonesha kuvutiwa na picha ya mwanamume mwingine.

Mtukufu Mtume (s.a.w.w) alisema: “Mwanamke yeyote aliyeolewa ambaye huwatazama wanamume wengine atakabiliwa na adhabu kali ya Mwenyezi Mungu.”