پایگاه اطلاع رسانی آیت الله ابراهیم امینی قدس سره

Uwe Kama Mama Kwake

Uwe Kama Mama Kwake

Wakati wa kazi nyingi na kuumwa maradhi, mtu anahitaji kutunzwa na watu wengine. Muuguzi anaweza kusaidia kupona kwa mgonjwa vizuri mno kwa sababu ya kumwangalia mgonjwa kwa wema na mapenzi. Wanamume ni watoto wadogo ambao wamekuwa. Watahitaji matunzo kama ya mama. Mwanamume akioa mwanamke, anatarajia mke wake kuwa kama mama yake kwake wakati akiugua na matatizo.

Bibi mpendwa! Kama mume wako anaugua, muangalie zaidi kuliko ilivyo kawaida.

Onesha huruma yako kwake na uoneshe kwamba umefadhaishwa sana na ugonjwa wake huu. Mliwaze, tayarisha mahitaji yake yote na wanyamazishe watoto ili mgonjwa apumzike. Kama anahitaji daktari au dawa, basi fanya atakavyo. Mpikie chakula anacho kipenda na ambacho ni kizuri kwake. Muulize kuhusu afya yake mara kwa mara. Jaribu kukaa karibu naye kadiri iwezekanavyo. Kama anaumwa sana hivyo kwamba hawezi hata kupata usingizi na wewe usilale kadiri iwezekanavyo. Mara utakapo amka, mwendee.

Muulize hali yake inaendeleaje. Kama usiku huo hakulala kabisa, basi onesha masikitiko yako. Hakikisha chumba chake kipo kimya wakati wa mchana. Matunzo yako kwake yatasababisha mgonjwa kupata nafuu haraka. Atafurahia juhudi zako na kukupenda zaidi. Zaidi ya hayo angefanya hivyo kwako endapo ungeugua.

Mtume (s.a.w) wa Mwenyezi Mungu alisema: “Jihadi ya mwanamke ni kumtunza vizuri mume wake.”