پایگاه اطلاع رسانی آیت الله ابراهیم امینی قدس سره

Kama Mume Anafanya Kazi Nyumbani

Kama Mume Anafanya Kazi Nyumbani

Wanawake wale ambao waume zao wanafanya kazi nje wana uhuru nyumbani. Lakini baadhi ya wanaume wanafanya kazi nyumbani, kama vile watunzi wa mashairi, waandishi, mafundi rangi, au wanasayansi ambao huhitaji kusoma sana. Wake wa wanaume wa aina hii wana uhuru mdogo nyumbani na kwa hiyo maisha yao ni tofauti.

Kazi zilizotajwa hapo juu zinahitaji umakini zaidi, kipaji na akili. Kwa hiyo, panahitajika faragha na ukimya. Saa moja ya kazi iliyofanywa mahali pa ukimya ni sawa na kazi iliyofanywa kwa saa kadhaa mahali penye shughuli na kelele nyingi. Tatizo liko wazi kwa upande moja, mwanaume anahitaji mahali palipo tulia afanye kazi yake na kwa upande mwingine, mke anataka apite hapa na pale ndani ya nyumba kwa uhuru.

Kama mwanamke anapanga mambo ya nyumba kama hiyo kwa namna ambayo kwamba mume wake anaweza kuendelea na kazi yake, kwa kweli atakuwa amefanikisha kazi ya manufaa. Mafanikio ya aina hiyo kwa hakika hayapatikani kwa urahisi, hususan pale ambapo wapo watoto. Lakini, hata hivyo, tatizo lazima litatuliwe, kwa sababu maendeleo ya mume katika kazi yake yatategemea kutokuwepo kwa tatizo hili.

Kama mwanamke anashirikiana na mume wake, anaweza kumfanya awe mtu wa kuheshimiwa ambaye atakuwa na sifa kwake na jamii.

Mwanamke ambaye mume wake hufanya shughuli zake nyumbani, asije akamtarajia kumlea mtoto, kufungua mlango kwa ajili ya wageni, kwenda jikoni, kusaidia kazi za nyumbani, kukemea watoto…Lakini anatakiwa afikirie kana kwamba hayupo ndani ya nyumba ambapo anaendelea na kazi.

Mpendwa Bibi! Mume wako anapotaka kwenda chumba cha kusomea tayarisha kalamu, karatasi, sigara, kisahani cha majivu, kiberiti, vitabu na vitu vingine atakavyo vihitaji.

Ukishatayarisha chumba na vitu anavyo vihitaji, mwache peke yake. Usizungumze kwa sauti kubwa na usiwaruhusu watoto wapige kelele. Wafundishe watoto wako wasicheze kwa fujo na kelele wakati baba yao anaendelea na kazi. Usiseme naye kuhusu mambo ya kila siku. Jibu hodi ya mlangoni na simu. Kama mtu anataka kumuona au kuzungumza naye mwambie anashughuli. Wakirimu wageni wakati anapopumzika.

Waambie marafiki na ndugu zako kumtembelea mume wako wakati hana shughuli. Marafiki zako wa kweli hawataudhika kwa taarifa yako hiyo. Wakati unafanya kazi zako za nyumbani, mtekelezee mahitaji yake, usimwingilie kati.

Labda baadhi ya wanawake wanafikiri haiwezekani kuishi kwa njia hii. Wanaweza wakasema: “Hivi inawezekana mwanamke kufanya kazi ngumu ya nyumbani na wakati huo huo amtunze mume wake pasipo kuruhusu kitu chochote kuingilia kazi zake?”

Ni kweli kwamba maisha ya aina hii si ya kawaida na huonekana magumu, lakini kama wanawake wahusika wanatafakari kuhusu umuhimu wa kazi za waume zao, wanaweza kuamua kutatua tatizo kwa kufanya mpango, bidii na hekima. Upekee wa baadhi ya wanawake hudhihirika katika hali kama hii. Vinginevyo, kuendesha maisha ya familia ya kawaida ni kazi ya kawaida.

Mpendwa Bibi! Kuandika kitabu, makala nzuri ya kisayansi au tungo nzuri, kuandika shairi zuri sana, kutengeneza mchoro mzuri au kutatua matatizo ya kisayansi si kazi rahisi. Lakini, moyo kwa upendo na ushirikiano, hilo linawezekana.

Je, huko tayari kuyatoa mhanga matamanio yako pamoja na mabadiliko kidogo tu katika maisha yako? Kwa kufanya hivyo utakuwa unamsaidia mume wako katika kazi yake. Kwa msaada wako huo, mume wako atapata hadhi kubwa na wewe utashiriki katika hadhi hiyo.