پایگاه اطلاع رسانی آیت الله ابراهیم امینی قدس سره

Samehe Makosa Ya Mumeo

Samehe Makosa Ya Mumeo


Kila mtu isipokuwa wale ambao Mwenyezi Mungu amewatangaza kuwa


‘Maasum’


hufanya makosa. Watu wawili wanaopendana na wanashirikiana pamoja, hufanya makosa, lazima wawe wasemehevu. Kama hawatasameheana, basi ndoa yao itavunjika.

Wafanya biashara wawili ambao ni wabia, na jirani wawili, marafiki wawili na hususan mume na mke wanahitaji kusameheana.

Kama watu wa familia hawasameheani na kufuatilia makosa ya kila mmoja wao, basi ama familia itafarakana au wataishi maisha yasiyovumilika.

Mpendwa Bibi! Pengine mumeo hufanya makosa. Anaweza akakutukana, akakufedhehesha, akasema uwongo, anaweza hata kukupiga. Matendo kama hayo yanaweza kufanywa na mwanamume yeyote.

Baada ya kufanya kosa, kama mumeo hujuta kwa kosa hilo au wewe unahisi anajuta kwa kosa lake hilo, basi msamehe na usilifuatilie jambo hilo. Kama anajuta lakini hayupo tayari kuomba msamaha, basi usijaribu kuthibitisha kosa lake. Vinginevyo, anaweza kuhisi anadhalilishwa na anaweza kulipiza kisasi kwa kukumbuka makosa yako na kwa hiyo, ikawa chanzo cha ugomvi mkubwa kwa hali hiyo, ni bora wewe unyamaze kimya hadi hapo atakapo jilaani mwenyewe kutoka kwenye dhamira yake na akaanza kuhisi majuto kuhusu kosa hilo. Hapo atakuona wewe kuwa ni mtu mwenye busara na mke wa kujitoa kwa mambo mema ambaye anavutiwa na mume wake, na familia yake.

Mtume (s.a.w.w) wa Mwenyezi Mungu alisema: Mwanamke mbaya hatoi msamaha kwa makosa ya mumewe na hakubali hata kuomba msamaha.”

Je, si ni jambo la kusikitisha kwamba mkataba wa ndoa takatifu unavunjwa kwa sababu mwanamke hayupo tayari kusamehe makosa fulani ya muewe?