پایگاه اطلاع رسانی آیت الله ابراهیم امینی قدس سره

Kuwa Mwangalifu Mume Wako Asipotoshwe

Kuwa Mwangalifu Mume Wako Asipotoshwe

Wanaume wanatakiwa kuwa na uhuru wao na ushirikiano wao katika shughuli ili waweze kufanya kazi na kuendelea kwa namna inayowafaa. Kama wanaume watawekewa masharti katika shughuli zao, basi, hawatakuwa na furaha. Mke mwenye busara hawezi kuingilia mambo ya mume wake.

Mke hatakiwi kufuatilia nyendo za mume wake; kwa sababu lazima atambue kwamba kwa kumnyima mume wake uhuru anaouhitaji na kujaribu kumdhibiti katika shughuli zake anaweza kujibu kwa ukali sana.

Wanaume wenye busara na uzoefu hawahitaji kudhibitiwa.Wanaume kama hao kila mara kufanya mambo yao kwa busara; si rahisi kuwa danganya; wao wanawajua marafiki zao na maadui zao. Hata hivyo, wapo watu ambao ni wa kawaida; watu hawa wanaweza kudanganywa kwa urahisi na kuvutiwa kwa urahisi na watu wengine.

Wapo watu ambao ni laghai na wanangoja kuwadanganya watu wa kawaida. Mtu laghai, licha ya kujifanya kuwa mwema, humtega na kumnasa mtu mwingine na kumwelekeza kwenye uovu. Jamii iliyojaa uovu na tabia ya binadamu isiyokubali kushindwa haisaidii kurekebisha hali. Mtu wa kawaida anaweza asijue hali yake kwa kipindi fulani, lakini siku moja anashtuka na kujikuta yupo kwenye kina cha mtego na hawezi kujinasua.

Ukiangalia kila mahali pale ulipo, utaona watu wengi wa aina hiyo wenye bahati mbaya. labda hakuna hata mmojawao aliye nuia kuanguka kwenye mtego au kuwa mwovu. Lakini kupitia kwa urahisi wao, ujinga na uamuzi wa pupa sasa wamekuwa mawindo ya waovu katika jamii.

Kwa sababu hii, watu wepesi wanatakiwa kusimamiwa. Kwa kufuatilia shughuli zao, watu wenye busara na wenye kuwatakia mema wenzao watakuwa wamewafanyia huduma kubwa.

Watu wazuri sana kwa kazi hii, hata hivyo, ni wake wa wanaume hawa. Mke mwenye busara na mwerevu anaweza kufanikiwa kazi kubwa sana kuhusu mume wake, kwa msimamo wa kumsaidia na busara.

Wanawake wa aina hii, hata hivyo, lazima wakumbuke kwamba hawatakiwi kuingilia moja kwa moja mambo ya waume zao, au kuwaambia “Wafanye hivi” na “wasifanye vile”. Sababu yake ni kwamba wanaume mara nyingi hawataki kabisa kutumiwa kama kitendea kazi mikononi mwa wengine vinginevyo watajibu kwa ukali. Lakini mwanamke mwenye hekima angefuatilia shughuli za mumewe na kuwaangalia washirika wake bila kudhihirika, na mume asitambue.

Pia hutokea kwamba baadhi ya wanamume, wakati mwingine huchelewa kurudi nyumbani isivyo kawaida. Endapo jambo hili linatokea na idadi ya siku anazochelewa kurudi nyumbani imo katika kiwango kinacho kubalika, basi hapana haja ya kuwa na wasi wasi, kwa sababu upo wakati ambapo wanaume hujikuta wanajaribu kushughulikia mambo ambayo hawakuyategemea baada ya kazi zao. Hata hivyo, endapo idadi ya siku anazochelewa kurudi nyumbani inazidi kiwango kisicho kubalika, basi, mke wake atalazimika kufanya upelelezi. Lakini, upelelezi si jambo rahisi, unahitaji uvumilivu na busara, mtu lazima aepuke hasara na malalamiko.

Kwanza kabisa, mke anatakiwa azungumze na mume wake kwa upole na wema: Mke amuulize mume wake kwa nini alirudi nyumbani kwa kuchelewa kuliko jana yake na alikuwa wapi. Mke anatakiwa kufuatitilia jambo hili kwa busara na uvumilivu katika nyakati mbali mbali na fursa tofauti. Kama atagundua kwamba mumewe huchelewa kurudi nyumbani kwa sababu ya kazi yake au kuhudhuria mkutano wa kisayansi, kidini na kimaadili, basi amwache aendelee hivyo. Kama mke anahisi kwamba mume wake amepata rafiki mpya, anatakiwa ajue rafiki huyoni nani. Kama rafiki yake mpya ni mtu mwenye tabia njema na mwenendo safi, basi, asiwe na wasi wasi, kwa sababu rafiki mzuri ni neema kubwa.

Ukihisi kwamba mume wako anaingia kwenye upotofu au ameshirikiana na watu waovu na wasiofaa, basi unatakiwa umsitishe haraka sana. Katika hali kama hii, mwanamke anao wajibu mkubwa sana.

Kosa dogo tu katika kushughulikia jambo hili, kwa kufanya uzembe, linaweza kuharibu maisha ya familia yao.

Hii ni hali ambapo busara na werevu wa baadhi ya wanawake hutumika na kudhihiri. Mtu lazima akumbuke kwamba ugomvi na ubishi si suluhu na huweza kusababisha kinyume chake. Mwanamke nayepitia kwenye tukio hili anazo kazi mbili za kufanikisha: kwanza anatakiwa kutathmini hali ya nyumbani; na ajipime yeye mwenyewe na msimamo wake. Lazima agundue sababu ya tabia ya mume wake.

Lazima afanye uamuzi usio na upendeleo kwa nini haoneshi uchangamfu kwa familia yake na kuelekea kwenye upotofu. Mke anaweza akang’amua kwamba msimamo wake mwenyewe ndio umekuwa sababu; au labda alikuwa ndio sababu; au labda alikuwa hajali vyakula anavyo vipenda mumewe, jinsi anavyoonekana au mambo ya nyumbani. Mambo kama haya huwafanya wanaume wafarakane na familia. Wanaweza wakafuatilia mambo ya upotofu ya nje ili wasahau matatizo yao. Mke anaweza kumuuliza mume wake kuhusu matatizo yake na ajaribu kusaidia kuyatatua.

Kama mwanamke alijisahihisha na kuibadilisha nyumba kulingana na matakwa yake, basi, awe na matumaini kwamba mume wake atarudi tena kwenye familia yake na kwamba ataepuka sehemu zenye uovu.

Pili, mke lazima amwoneshe mume wake wema mwingi kadiri iwezekanavyo. Lazima amshauri mume wake na kumkumbusha matokeo mabaya na matendo yake. Anaweza hata kulia na kumwambia awaache marafiki zake wabaya. Lazima amwambie: Nina kupenda kwa dhati ya moyo wangu. Ninajivuna kuwa na wewe. Ninaona heri kuwa na wewe kuliko vitu vyote na nipo tayari kujitolea kwa ajili yako. Lakini nina huzunishwa na kitu kimoja; kwa nini mwanamume kama wewe, awe na marafiki kama, au ahudhurie dhifa ya aina hiyo? Matendo kama haya hayastahili kufanywa na wewe. Tafadhali acha kufanya mambo haya.

Mke lazima aendelee na msimamo huu hadi aushinde moyo wa mume wake. Inawezekana kwamba mume amezoea kuendekeza tabia zisizofaa na kwamba hawezi kuathiriwa kwa urahisi, lakini mke asikasirike. Lazima afuatilie lengo lake kwa juhudi na uvumilivu zaidi.

Wanawake wanao uwezo mkubwa kwa wanaume. Mwanamke anaweza kufanya lolote atakalo kama akili yake itamwelekeza kufanya hivyo. Kama mwanamke anaamua kumwokoa mume wake kutoka kwenye kinyaa cha maovu, anaweza kufanya hivyo. Upo uwezekano wa asili mia themanini kushinda, almuradi utekelezaji wake uwe wa busara. Kwa vyovyote vile, mke hatakiwi kutumia nguvu au msimamo wa ukali; isipokuwa tu kama haoni matokeo yoyote ya kuonesha wema na upole kwake. hata hivyo, hatakiwi agombane, aondoke nyumbani au atumie njia nyingine yoyote ile ya upole kadiri iwezekanavyo na si kulipize kisasi.

Ndio, kutunza mume ni kazi ya kila mke. Ni kazi ngumu na ndio maana Mtume (s.a.w) alisema: “Jihadi ya mwanamke ni kumtunza mume ipasavyo.”