پایگاه اطلاع رسانی آیت الله ابراهیم امینی قدس سره

Ujauzito Na Kuzaliwa Mtoto

Ujauzito Na Kuzaliwa Mtoto

Muda wa kudumu ujauzito ni kipindi nyeti chenye matukio ya majaliwa kwa maisha ya mtoto. Tabia ya lishe ya mama pamoja na harakati za kimwili na za kisaikolojia ni mambo ya muhimu kwake na maisha ya kimbe kilichomo kwenye tumbo lake la uzazi.

Afya au maradhi ya mtoto, nguvu au udhaifu, ubaya wa sura au uzuri wa sura na tabia yake nzuri au mbaya na sehemu ya akili na busara, huanzishwa kwenye tumbo la uzazi la mama. Mmoja wapo wa wataalamu ameandika: “Wazazi wa watoto ama wanaweza kukua kwenye ngome ya afya au kwenye uharibifu wa maradhi. Ni wazi kwamba uharibifu wa maradhi si sehemu inayofaa kuishi roho ya milele au mwanadamu. Hii ni sababu ambayo kwamba wazazi wanaaminika kubeba wajibu mkubwa sana ikilinganishwa na uumbaji wote.”

Kwa hiyo, kipindi cha mimba hakiwezi kufikiriwa au kufanywa kama cha kawaida. Mara tu mimba inapoanza, wazazi hupewa wajibu mkubwa.

Wazazi wanaweza bila kufahamu kusababisha matatizo ya aina nyingi, yaliyo mengi baina yao yanaweza kuwa magumu sana kurekebishwa, kwa sababu ya uzembe mdogo wakati wanapofanya kazi zao.

Yafuatayo ni mambo ambayoyanayofaa kuangaliwa: Chakula: Kilengwa kilichomo kwenye tumbo la uzazi la mama yake, hula chakula na kukua kwa lishe ya damu yake. Kwa hiyo, chakula cha mama kinatakiwa kuwa na virutubishi vya kutosha ili viweze kumpa mtoto vitu vya asili anavyo vihitaji, pia kwa ajili ya ustawi wa mama. Kwa hiyo, upungufu wowote wa vitamini, protini, mafuta, sukari au wanga katika ulaji wa mama inaweza kusababisha madhara katika afya ya mtoto. Imam Sadiq (a.s) alisema: “Chakula cha kilengwa kinapatikana kwenye lishe anayopata mama.” 256.

Tatizo kubwa ambalo linawapata wanawake wengi sana wajawazito ama katika kipindi fulani cha ujauzito au kipindi kikubwa cha ujauzito, hupungukiwa na ladha ya lishe bora, kwani hupatwa tabia ya tamaa ya vyakula fulani huku akisikia kinyaa kwa vyakula vingine.

Kwa sababu kawaida hula chakula kidogo wakati wa kipindi hiki, lazima wahakikishe kwamba chakula chao si kizito na wakati huo huo kiwe na virutubisho vya kutosha ili kiweze kumpa mtoto vitu vya msingi.

Ufuatiliaji wa mpangilio ya chakula katika kipindi hiki cha ujauzito ni mgumu sana, hususan kwa watu wasio na uwezo wa kifedha na wale ambao hawana ujuzi wa ubora wa vyakula mbali mbali. Wajibu mkubwa anao baba ambaye anatakiwa kufanya jitihada kubwa kutoa vyakula vya msingi kwa mke wake. Kutokujali kwa upande wa baba kungeweza kusababisha madhara kwa mtoto anayekua, ambapo yeye ndiye atakaye wajibishwa hapa duniani na akhera.

Hali ya kiakili: Mama, wakati wa ujauzito anahitaji utulivu na anatakiwa apate hisia ya uzoefu wa kupenda maisha. Hii ina faida kwa mama na mtoto wake. Baba akiwa ni mwenye wajibu wa kumpa mke wake mazingira ya amani na uchangamfu, lazima ajaribu kwa bidii zaidi wakati wa kipindi cha ujauzito wake. Mume kwa wema na upendo, anatakiwa kuwa na mwenendo kwa namna ambayo mke wake anaweza kujivuna na kufurahi kuhusu yeye kuwa na ujauzito, lazima aone fahari kwamba maisha ya kiumbe kingine yanategemea kwake na kwamba anawajibu wa ustawi wake.

Mjamzito aache miondoko ya kushtua. Mwanamke mwenye mimba anatakiwa kuepuka shughuli nzito na anatakiwa kupumzika sana. Kunyanyua kitu kizito au miondoko ya haraka ya mwili inaweza kusababisha madhara yasiyo rekebika kwake, mtoto au wote. Wanawake wajawazito wanatakiwa kuepuka kazi ngumu na waume zao wanatakiwa kujitolea kufanya kazi kama hizo.

Woga wa uchungu wa Kujifungua. Kujifungua mtoto mara nyingi huwa si kazi nyepesi. Maumivu ya uchungu wa kujifungua wakati mwingine huwa makali sana.

Wanawake wajawazito mara nyingi huwa na wasi wasi kuhusu maumivu yaliyomo na uwezekani wa hatari yanayohusishwa na kujifungua mtoto, inayofuatiwa na kipindi cha kupata ahueni baada ya kujifungua. Ingawa wanawake wanatakiwa kustahamili ujauzito, uchungu wa kujifungua na kulisha watoto wao, wanamume pia wanatakiwa kugawana wajibu wa kulea watoto wao.

Ingawa kiinitete kinatungwa kwenye tumbo la uzazi la mwanamke pia yupo baba wa mtoto ambaye amefanya kazi muhimu katika kutungwa mimba. Kwa hiyo, wanamume wanatakiwa kuhakikisha kwamba wake zao wanapata maliwazo wakati wa kujifungua na kuwa tayari kusaidia endapo chochote kitahitajika haraka.

Ni kazi ya kibinadamu na kiislamu kwa wanaume kufanya kila wawezalo kwa wake zao wajawazito kwa kuwapa matunzo ya kitabibu na mahitaji ya kurahisisha kujifungua. Mwanaume anatakiwa kuwa na mke wake baada ya kuzaliwa kwa mtoto, lakini kama hawezi kufanya hivyo anatakiwa ampigie simu au amtumie ndugu zake wakae naye. Anatakiwa kujaribu kumrudisha nyumbani yeye mwenyewe na amsaidie kufanya kazi za nyumbani ili mke wake apate mapumziko ya kutosha na kurudisha tena nguvu iliyopotea. mwanaume anaye mfanyia mke wake wema, atazawadiwa na Mwenyezi Mungu. Mtume (s.a.w.w) alisema: “Mwanaume aliye mbora sana miongoni mwenu ni yule anayemfanyia mke wake wema.

Na mimi miongoni mwenu ni mwanaume mbora sana kuhusu kuwafanyia wema wake zangu.”

Imamu Sadiq (a.s) alisema: “Mwenyezi Mungu na amrehemu mwanaume ambaye kufanya uhusiano mzuri na mke wake, kwa sababu Mwenyezi Mungu anamteua mwanaume kuwa mlezi wa mke wake.”

Mwanaume anaye mtendea mke wake wema, atafanya mazingira ya familia yake kuwa machangamfu na ataimarisha misingi yake. Mke wake, kwa upande wake, kamwe hatasahau mapenzi ya mume wake na huba yake. Matokeo yake mshikamano wa ndoa unakuwa imara zaidi.