پایگاه اطلاع رسانی آیت الله ابراهیم امینی قدس سره

Pia Uwe Msafi Nyumbani

Pia Uwe Msafi Nyumbani

Kufuata kanuni za usafi kwa kila mtu na kila mahali ni muhimu. Mtu lazima aweke mwili wake na nguo zake katika hali ya usafi, wakati wote. Lazima aoge angalau mara moja kwa wiki na lazima aoshe uso wake na mikono yake kwa sabuni, achane nywele zake, anyoe nywele, aoshe miguu yake, avae soksi safi kila siku na lazima pia avae nguo zenye tohara. Dini tukufu ya Uislamu inasisitiza sana kuhusu usafi na kuvaa vizuri.

Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w) alisema: “Usafi ni sehemu ya imani (ya Uislamu).”

Mtukufu Mtume (s.a.w.w) alimuona mtu aliyekuwa mchafu, nywele zake hazikuchanwa na yeye hakuwa katika hali ya kuvutia. Mtume (s.a.w.w) alisema: “Kutumia neema za Mwenyezi Mungu ni sehemu ya imani ya Uislamu.”

Mtume (s.a.w) wa uislamu pia alisema: “Mtu mchafu atakuwa mfanya ibada mchafu wa Mwenyezi Mungu.”

Mtukufu Mtume (s.a.w.w) aliongeza kwa kusema: “Jibril alisisitiza sana kupiga mswaki meno hivyo kwamba nikawa nayahofia.”

Imamu Ali (a.s) alisema: “Mwenyezi Mungu ni mzuri na hupenda uzuri. Na pia hupenda kuona athari za neema Zake zinapotumiwa na waja wake.”

Usafi na uzuri si kwa ajili ya wanawake tu, lakini wanaume lazima pia wanatakiwa kuwa safi na wavae vizuri. Baadhi ya wanaume hawajali usafi wao na huoga mara moja kwa kipindi fulani. Hawajali nguo zao zipo katika hali gani na hawajali hata kunyoa ndevu zao. Wananuka harufu mbaya sana hivyo kwamba huwafanya wengine kuwa mbali nao.

Wanaume ambao ni waangalifu kuhusu usafi na huweka umuhimu kuhusu nguo zao, mara nyingi hufanya hivyo nje ya nyumba zao. Ni kwamba wanaonekana safi na kuvaa vizuri nje ya nyumba kwa ajili ya watu, si ndani ya nyumba zao kwa ajili ya familia zao. Huonekana nadhifu sana mitaani, kwenye mikusanyiko na kadhalika lakini mara tu wanaporudi nyumbani; huvaa nguo zilizochakaa. Mara chache sana kuangalia hali ya nywele zao na nyuso zao wanapokuwa nyumbani kwa ajili ya familia zao.

Wanaweza hata wasijali kunawa uso kabla ya kunywa chai ya asubuhi. Wanaume wa aina hii huzifanya familia zao zisiwajali.

Bwana mpendwa! Kama huwezi kumvumilia mke aliye mchafu na aliye vaa nguo zilizo chakaa na unatarajia aonekane safi na mzuri akiwa nyumbani, basi uwe na uhakika kwamba anatarajia hivyo hivyo kutoka upande wako. Mkeo pia, huchukia mume mchafu, anaye nuka na asiye nadhifu. Mke wako anataka kukuona wewe katika hali safi na nadhifu.

Kama utashindwa kutosheleza matarajio yake kuhusu unadhifu, anaweza akawaona wanaume wengine ambao wanaonekana safi na nadhifu na anaweza hata kudhani kwamba wametokea dunia nyingine. Atakulinganisha na wao na yawezekana akapoteza mvuto kwako. Kwa nini unaonekana safi kwa ajili ya wageni huko mitaani lakini unaonekana mchafu mbele ya mke wako na watoto wako.

Kwa hiyo, dini tukufu ya Uislamu inawaamuru wanamume wajipambe mbele ya wake zao.

Mtume (s.a.w.w) wa Uislamu alisema: “Ni wajibu kwa mwanaume kumpa mke wake chakula na nguo na asionekane mbele yake akiwa mchafu na hapendezi. Kama angetimiza yaliyotajwa hapo juu, haitamwia vigumu kutekeleza haki za mke wake.”

Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w) pia alisema: “Enyi wanamume lazima mjiweke katika hali ya usafi na kuweni tayari kwa wake zenu kama ambavyo nyingi mnavyotaka wake zenu kuwa tayari kwa ajili yenu.”

Hasan bin Jiham anasema: “Nilimuona Hadhrat Abu al-Hasan (a.s) ambaye alipaka rangi nywele zake. Niliuliza kama kweli alipaka rangi nywele zake” Alisema: ‘Ndio, mapambo ya mwanamume kwa ajili ya mke wake kusaidia kumweka mke katika uaminifu. Wanawake wanaoacha njia safi na kuanza kufanya uovu ni kwa sababu ya uzembe na makosa ya waume zao.’ Hadhrat Abu al-Hasan alisema: ‘Unapenda kumuona mke wako katika hali ya uchafu?’ Nilijibu: ‘Hapana’ Halafu akaongezea: ‘Hufikiria kama unavyo fikiria wewe.’ ” Imamu Rida (a.s) alisema: “Wanawake wa Bani Israel waliacha njia iliyosafi kwa sababu waume zao hawakujali usafi wao na unadhifu wao.” Halafu Imamu akaongeza: “Vile unavyo mtarajia mke wako, ndivyo anavyotarajia kwako.”