پایگاه اطلاع رسانی آیت الله ابراهیم امینی قدس سره

Uwe Msikivu

Uwe Msikivu

Mwanamke ni kiumbe mwenye hisia kubwa ambazo hutawala mantiki yake. Mwanamke ni mjinga na mwepesi kuhisi kuliko mwanamume. Mwanamke anaweza kudanganywa kwa urahisi zaidi na hawezi kudhibiti matashi ya hisia zake. Hawezi kuamua kwa busara pindi anapotibuliwa. Anaweza kufurahishwa au kutibuliwa kwa urahisi sana.

Hivyo kama mwanaume ana usimamizi wa tabia na matendo ya mke wake, hatari za watu wengi zingeepukwa.

Ndio sababu dini tukufu ya Uislamu imemteua mwanamume kuwa kama mlezi wa familia yao na hufanya kuwa na wajibu kwa mambo ya familia.

Mwenyezi Mungu anasema kwenye Qurani Tukufu:

الرِّجَالُ قَوَّامُونَ عَلَى النِّسَاءِ بِمَا فَضَّلَ اللَّهُ بَعْضَهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ وَبِمَا أَنْفَقُوا مِنْ أَمْوَالِهِمْ ۚ فَالصَّالِحَاتُ قَانِتَاتٌ حَافِظَاتٌ لِلْغَیْبِ بِمَا حَفِظَ اللَّهُ
 

“Wanamume ni wasimamizi wa wanawake kwa kufadhiliwa na Mwenyezi Mungu baadhi yao juu ya baadhi, na kwa mali yao wanayo yatoa. Basi wanawake wema ni wale wenye kutii na wanao jitihada hata katika siri kwa kuwa Mwenyezi Mungu ameamrisha wajilinde.”
(Quran 4:34).
Kwa hiyo mwanaume anayeonekana kama mlinzi wa familia yake, asifanye uzembe kuhusu matendo ya mke wake. Kila mara lazima afawidhi mambo ya mke wake na kufuatilia matendo yake. Lazima mume ahakikishe kwamba mke wake hapotoki au kujumuika na aina ya watu wabaya.

Mume lazima amweleze mke wake kimantiki kuhusu madhara ya rafiki mbaya. Asimruhusu kuondoka nyumbani akiwa amevaa nguo zisizofaa au zile zinazosababisha ashiki ya kijinsia. Asimruhusu mke wake ashiriki kwenye shughuli ovu au kuhudhuria mikutano isiyofaa.

Ni kweli kwamba kama mwanamke akiachwa peke yake katika matendo yake na kuchanganyikana na watu, inawezekana akanasa kwenye mtego wa watu wenye akili potovu na huishia kwenye upotovu.

Wanaume wanashauriwa kuangalia idadi ya wanawake ambao kwa sababu ya uzembe wa waume wao wamenasa kwenye mtego wa uovu. Wapo wanawake wengi ambao wamedanganywa kwenye karamu za usiku. Familia nyingi zimevunjika na watoto wengi wamepoteza familia zao. Kwa sababu ya mikusanyiko hiyo.

Mwanaume anaye mruhusu mke wake kuondoka nyumbani akiwa amevaa nguo zisizofaa, kuwa na marafiki wabaya na hamzuii kuhudhuria mikusanyiko yenye uharibifu, kwa kweli atakuwa anafanya kosa kubwa sana la uhaini kwake, kwa mke wake na kwa watoto wake.

Msimamo huu ungemwelekeza mke wake kwenye mamia ya sehemu za hatari ambamo hawezi kujinasua kwa urahisi. Petroli hushika moto kwa urahisi sana, kwa hiyo ni tendo la kipumbavu kuacha petroli karibu na moto na kudhani kwamba haitashika moto.

Ujinga ulioje wa watu ambao huwaruhusu wake zao au mabinti zao kujionesha mitaani huku wakiwa wanavaa nguo zisizofaa na wakati huo huo hawapendi nadhari au kutupiwa macho na wanaume kwa sababu ya mavazi yao!

Uhuru usio sahihi wa aina hii unayo matokeo mabaya sana. Kama mwanamke amefaulu kumshinda mume wake kuhusu matamanio yake yasiyo halali, ataongeza matakwa hayo hadi kwenye kiwango ambacho atafanya mambo yake kwa uhuru bila kumjali mume wake. Hii itasababisha matukio ya uovu kwenye familia.

Ndio maana Mtume (s.a.w.w) alisema: “Mwanaume ni mlezi wa familia yake na mlezi yeyote anao wajibu kwa wale walio chini kuwatimizia mahitaji yao.”

Mtume (s.a.w.w) pia alisema: “Waamrisheni wanawake kufanya mema kabla hawajakufanyieni ninyi uovu.”

Kwa nyongeza Mtume alisema: “yeyote anaye mtii mke wake, Mwenyezi Mungu atamtupa kwenye moto akitanguliza uso wake.”

Mtume aliulizwa: “Aina gani ya utiifu unaomaanishwa hapa?” Mtume

(s.a.w.w) alijibu: “Ni hapo ambapo mume humruhusu mwanamke ambaye humwomba mume wake ruhusa ya kwenda kwenye hamamu ya nje, watu kuhudhuria harusi, sherehe na mikusanyiko ya kutoa rambi rambi akiwa amevaa nguo za kumfedhehesha.”

Imamu Sadiq (a.s) alisema: “Furaha kamili ya mwanaume ni kwamba awe mfawidhi na kiongozi wa familia yake.”

Mtume (s.a.w.w) wa Uislamu alisema: “Mtu yeyote anayemruhusu mke wake ambaye amejipamba, kuondoka nyumbani kwake ni mtu mwenye roho ya kikatili na yeyote atakaye mwita hivyo, atakuwa hakufanya dhambi.

Na mwanamke yeyote ambaye mume wake humruhusu kutoka nyumbani kwake akiwa amejipamba na kujipulizia manukato, kila hatua atakayo tembea, Mwenyezi Mungu atamjengea nyumba mume wake huyo katika Jahannamu.”

mwisho ninawakumbusha kuhusu mambo mawili: Ni sahihi kwamba mwanaume anatakiwa kuwa na hadhari kwa mke wake lakini zoezi hili linatakiwa kufanywa kwa uangalifu na busara. Mume hatakiwi kukimbilia kukasirika au matumizi ya nguvu. Asimwoneshe mke wake kwamba anaamuriwa au vinginevyo atatoa jibu kwa njia isiyopendeza. Njia iliyo nzuri kabisa, kwa mwanaume ni kuwa na huruma na uelewa. Lazima atekeleze zoezi hili kama mwenza mwenye upole na amwambie mke wake kuhusu madhara ya matendo maovu. Lazima atengenezewe mazingira ya kuchagua njia iliyo nyooka yeye mwenyewe kwa shauku na hamu.

Mwanaume anatakiwa kuwa na wastani, ni kwamba wala asiwe mkali sana na kiherehere ama asiwe mzembe.

Mwanamke, kama alivyo mwanaume, anahitaji uhuru na anatakiwa apewe uwezo wa kujiamulia la kufanya kwenye makundi yake kwa usawa unatakiwa.

Lazima mwanamke awe huru awe huru kuwasiliana na wazazi wake, kaka zake na dada zake, na lazima aruhusiwe kuwa na watu wa aina inayofaa.

Kwa ufupi, ipo mifano isiyo ya kawaida ambapo mwanamke ananyang’anywa utashi wake. Lakini hata kwenye mifano kama hiyo mtu hatakiwi kuvuka mpaka uliowekwa na kuwa mkali sana. Ukali wa kupita kiasi unayo madhara. Huharibu mazingira ya urafiki na husababisha maudhi. Mwanamke anaweza akajibu kwa ukali zaidi kutokana na ukali wa mume wake. Mke anaweza hata kuomba talaka.

Mwanamke kijana, mke wa… alimwambia mwandishi wa habari mahakamani: “Niliolewa na Bwana….Miaka mitano iliyopita. Tunao watoto wawili; mmoja wa kiume na mwingine wa kike. Wakati fulani mume wangu amekuwa anamchukulia kila mtu kwa namna ya ubeuzi. Haniruhusu mimi kushirikiana na mtu yeyote. Hata hufunga milango ya nyumba anapoondoka nyumbani. Sisi ni wafungwa ndani ya nyumba yake. Sasa, siwezi hata kwenda kwa wazazi wangu.

Watu wa familia yangu hawatutembelei, kwa sababu yake. Sijui nifanye nini! Kwa upande mmoja ni kwamba siwezi kuishi naye, na kwa upande mwingine, nina wasi wasi kuhusu hatima ya watoto. Kwa hiyo, niliamua kuleta shauri langu kwenye mahakama hii; labda wanaweza wakapitisha uamuzi fulani.”

Wanaume kama mume wa huyu mwanamke, kwa bahati mbaya ni wakali sana na si watu wa kawaida hivyo kwamba wake zao, licha ya kutaka kuishi pamoja na waume zao, huomba talaka. Wake zao huudhika sana, licha ya kuwa na watoto, wapo tayari kutengana nao.

Kwa nini mwanaume amkatae mke wake asishirikiane na ndugu zake wa karibu? Kwani haelewi kwamba ukali ukizidi kiasi, hutayarisha uwanja kwa baadhi ya wanawake kukengeuka? Kwani hajasikia au hajaona familia zilizosambaratika kutokana na tabia ya aina hii?

Hata kama mke wa mtu atavumilia ukali wa mtu, patakuwepo upungufu wa huba inayo changamsha mazingira ya familia ndani ya nyumba. Inawezekanaje mtu kutarajia mke aliyeko kifungoni kuwa mwema kwa mume wake na watoto au kufuatilia kazi za nyumbani kwa hamu?