پایگاه اطلاع رسانی آیت الله ابراهیم امینی قدس سره

Samehe Makosa Ya Mke Wako

Samehe Makosa Ya Mke Wako

mwanadamu aliyekamilika na sote sisi hufanya makosa mengi. Kama mambo yalivyo, hii ni kweli kwa wanamume na wanawake.

Kwa upande wa wanawake, anaweza kufanya makosa kwa kutokuwa na adabu kwa mume wake, kufanya kitu kinyume na matakwa yake kuwa mkali kwake, au kumwingiza kwenye hasara kiuchumi kwa sababu ya kuwa mzembe na kadhalika.

Kama mambo yalivyo, ni kweli kwamba wanandoa lazima waridhishane na waepuke kabisa kuudhiana wao kwa wao: Hata hivyo, hutokea mara chache kwamba mmoja wapo au wote watashindwa kukwepa kipengele hiki.

Baadhi ya wanaume hudhani kwamba wanatakiwa kuwa wakali kwa makosa ya wake zao kwa kuwa wanaamini hii kuwa ndio njia ya kuzuia kurudia kosa la aina hiyo.

Hata hivyo, uzoefu mara nyingi unaonesha matokeo kuwa kinyume chake kabisa. Mwanamke, ambaye mume wake ni mkali kwake, anaweza kuvumilia ukali wake kwa kipindi fulani, lakini hatimaye anaweza kuamua kujibu dhidi yake ikiwa kama matokeo ya kukatisha tamaa. Mke atazoea msimamo wake polepole hadi hapo atakapokuwa sugu.

Mume ambaye hatakuwa msamehevu kuhusu makosa ya mke wake, ni kwamba anamhamasisha mke wake kuwa jeuri na kukosa nidhamu. Anaweza kutaka kuendelea na msimamo huu ambapo kwa hakika atakabiliana na ugomvi mwingi wa mke wake. Wote wataishi katika hali ya uchungu kwa maisha yao yote.

Au anaweza akamwacha mke alivyo na asijihusishe naye kwa ukamilifu. Katika mfano huu mke wake, ambaye atahisi ameshinda, atakuwa hajali ridhaa na matakwa ya mume wake. Hali hii inaweza kufika kiasi kwamba hata hapo mke anapofanya makosa makubwa ya kudhamiria, atanyamaza. Hapo tena ndoa yao itakuwa imepoteza uchangamfu na wanaweza kukimbilia kutalikiana.

Kumbuka kwamba talaka husababisha madhara pande zote mbili kwa sababu kuanza maisha mapya si rahisi. Itakuwa hakuna uhakika wa kuwepo furaha baada ya kutalikiana.

Kwa hiyo, ukali haufai kutumika kila wakati na mara nyingi husababisha matukio yasiopendeza ambayo mtu anaweza kuyasoma kwenye magazeti. Njia nzuri kuliko zote ni kuwa mwenye kiasi na kutenda kimantiki. Samehe makosa yote madogo na yasio ya kukusudia yanayofanywa na mke wao. Hakuna haja ya kupiga kelele kwa ajili ya kosa la mke wako ambalo limefanyika bila kukusudia.

Kama mambo yalivyo, mara kwa mara mtu anaweza kuwashauri wenzake ili kuwasaidia wasirudie tena kosa la aina hiyo.

Watu hufanya makosa mengi kwa kutokujua, kwa hiyo ni vizuri zaidi kuwa shauri kwa uvumilivu kusahihisha matendo au maoni yao yaliyopotovu.

Kwa hiyo, mke wako hawezi kulazimishwa kurekebisha makosa yake; lakini badala yake unatakiwa kumpa maelezo kuhusu kosa, ili aweze kufanya uchaguzi, yeye mwenyewe asirudie tena kosa hilo.

Hivyo, si tu kwamba uelewano na kuheshimiana unabakia kama zamani, lakini pia kosa hilo litazuiwa na halitafanywa tena.

Ni busara kwa mwanamume kumzuia kimantiki mke wake asifanye makosa, lakini kama ataendelea kufanya makosa, basi kwa mara nyingine amsamehe na asijali makosa yake. Si rahisi kwa mume kuendelea kumpa adhabu mke wake au kujaribu kuonesha hatia yake ili amweke katika hali ya kuomba msamaha. Hii ni kwa sababu wanawake ni wajeuri kwa kawaida; na ukali usio stahili huwafanya watoe majibu zaidi kuliko ya hapo mwanzo. Hii inaweza kufatiwa na matukio yasiyopendeza na ya kuhofisha, kama vile kuachana au mauaji.

Uislamu umelielewa jambo hili nyeti, ambapo wanamume wamepewa wajibu kwa wanawake zao.

Imamu Ali (a.s) alisema: “Wavumilieni wanawake katika hali zote na semeni nao vizuri; na kwa kufanya hivyo wanaweza kurekebisha matendo yao”

Imamu Sajjad (a.s) alisema: “Ni haki ya mke wako kwamba unamtendea wema, kwa sababu yupo chini ya dhamana yako na unatakiwa kumlisha na kuvesha na unasamehe makosa yake ya kijinga.”

Imamu Sadiq (a.s) aliulizwa: “Mwanamke anazo haki gani kwa mume wake, ambazo kama akizitimiza ipasavyo, ataonekana kuwa mtu mwenye matendo mema?” Imamu alijibu: “Lazima ampe chakula na nguo na amsamehe makosa yake aliyoyafanya bila kukusudia.”

Imamu Sadiq (a.s) pia alisema; “Yeyote anaye waadhibu wale walioko chini yake, asitarajie kuheshimiwa au kupata cheo cha juu.”

Mojawapo ya sababu za ugomvi miongoni mwa wanamume na wanawake ni kwamba mama wakwe huingilia mambo ya familia zao.

Mama kabla ya kumuoza binti yake kwa mume, hudhani ya kwamba mkwilima wake kuwa mkamilifu na humthibitisha kwa binti yake kwamba ndiye atakaye mfanya awe na furaha. Atamheshimu na kumfanyia wema kwa matumaini ya kuwa na uwezo wa kurekebisha dosari zake ndogo ndogo baadaye.

Wakati mwingine mama mkwe humuona mkwilima wake hufuata matarajio yake na wakati mwingine hafuati. Katika mfano wa mwisho, anayo nia ya kumtengeneza mkwilima wake hadi hapo atakapo kubalika naye na katika utekelezaji wa hili hutumia kila njia zinazo wezekana kama vile za kwake mwenyewe na za uzoefu wa wengine na huanza kupanga namna ya kuwendea.

Wakati mwingine mama mkwe hujifanya mwenye huruma na wakati mwingine mkali. Anaweza akafanya mambo kama vile yeye ni mlezi na mfawidhi au anaweza akalalamika. Hata hivyo, chaguo zuri zaidi ni lile la kufanikisha lengo lake kwa kumvuta binti yake kwa kumfanya asifuate matakwa ya mume wake.

Huanza kumtumia binti yake na kwa hiyo humuamuru afanye tofauti nyakati mbali mbali. Kwa hiyo mwanaume humuona mke wake humlaumu leo na kesho kumuomba afanye kitu fulani.

Mwanamke mwenye uzoefu atafikiria kwamba mama angekuwa na huruma kuhusu ndoa yake na angefuata ushauri wake.

Hivyo kama mume wake hatafuata matakwa ya mama mkwe wake, ugomvi utaanza baina ya wanandoa na matokeo yake yanaweza kuwa kutalikiana au hata mauaji.

Hii ndio sababu wanamume wengi hawaelewani na mama wakwe zao. Huwalaumu kwa utovu wa adabu wa wake zao na huamini kwamba mama wakwe zao huwafundisha mabinti zao tabia mbaya.

Haitakuwa wazo mbaya kama mtu anajifunza kuhusu malalamiko ya wakwilima wachache.

Bwana M. Javda ameandika: “Mama mkwe wangu ni pepo mbaya, zimwi na joka la vichwa viwili. Mungu na amwepushe asiliwe na mbwa mwitu. Ameyafanya maisha yangu kuwa machungu sana hivyo kwamba ninapata wendawazimu na ninahisi kama vile nikimbie niende milimani na majangwani. Si mimi tu, ambaye nimechoshwa na hali hii. Huu ni mfano wa kawaida na ninadhani asilimia tisini na tano ya wanamume wana athiriwa na hawa mama wakwe na asilimia tano nyingine labda hawana mama wakwe.” Bwana F. Mohammed ameandika: “Mama mkwe wangu kila mara huingilia maisha yangu. Husababisha maudhi bila ya sababu ya maana. kila wakati husema maneno ya kashfa kuhusu familia yangu.

Wakati wowote ninaponunua kitu chochote kwa ajili ya mke wangu, mama mkwe wangu, huanza kuonesha dosari kuhusu kitu hicho. Hukosoa rangi yake au mtindo na hujaribu kuthibitisha kwamba kitu hakina thamani kwa mke wangu.” Bwana K. Parvis amendika: Mama mkwe wangu amenitendea kwa njia ambayo kwamba nimebakia kidogo nimtaliki mke wangu mara tatu. Huuma kama nge. Humfundisha mke wangu kuwa jeuri kwangu, kuacha kazi za nyumbani au kutarajia kisichowezekana kutoka kwangu. Wakati wowote anapokuja kututembelea, nyumba yetu hugeuka kuwa jahanamu. Kwa kweli sipendi hata kumuona.”

Wanaume wengi hujaribu kukabiliana na mvuto wa wakwe zao kwa wake zao kwa kuwekea mipaka uhusiano wao. Huwakataza wake zao wasiende kwa wazazi wao. Kwa ufupi, wanaume hawaelewani kabisa na mama wakwe zao na huonesha kutokupenda kwao kwa kila namna iwezekanayo.

Hata hivyo, mtazamo huu licha ya kwamba ni wa kawaida, si wenye mantiki na busara. Hii ni kwa sababu uhusiano wa mama na binti yake una nguvu sana na wa kimaumbile ambao hauwezi kuvunjwa kwa urahisi.

Inawezekanaje mwanaume kutarajia mke wake, kuwaacha wazazi wake ambao walitumia miaka mingi kumlea?

Matumanini haya hayatekelezeki na hata kama inatokea itakuwa kwa muda mfupi tu, kama ilivyo kwamba tendo lolote lisilo la kawaida halidumu muda wote.

Zaidi ya hayo kama mwanamke anahisi kwamba mume wake hawapendi wazazi wake, anaweza kuchukua msimamo kama huo kuhusu familia ya mume wake. Anaweza akawa hamtii, hamheshimu na kadhalika.

Juu ya hayo, msimamo huu wa mwanaume hutoa mwanya wa kisingizio kwa mama mkwe wake huingilia ndoa yake kwa ukali zaidi. Kwa ufupi, msimamo huu unaweza kusababisha matokeo mabaya na huenda yakawaelekeza wanandoa kutalikiana.

Kwa vyovyote vile kwa nini mwanaume ambaye anaweza kufaidika kutokana na kuelewana na wazazi wa mke wake, akimbilie hatua ya aina hiyo ambayo inaweza kumdhuru yeye na familia yake?

Mamlaka ya polisi wa India yalitoa taarifa kwamba mnamo mwaka 1971, sababu kubwa ya idadi ya matukio 146 ya watu kujiua wenyewe katika jiji la New Delhi ilikuwa uhusiano mbaya baina ya waume na mama wakwe zao.”

Mwanaume ambaye alikatishwa tamaa na mama mkwe wake kwa sababu ya kujiingiza kwake, alimtupa nje ya teksi.”

Mwanaume alivunja fuu la mama mkwe wake kwa nyundo. halafu kaka wa huyo mtu akakasirika na baada ya kumjeruhi kwa kisu akatoroka na kupotea.”

“Bwana…ambaye alikasirishwa na mama mkwe wake, alimwagia supu ya moto kichwani. Mama mkwe alipiga kelele na kupoteza fahamu. Alipelekwa hospitalini baada ya kupona akasema kwamba binti yake amemwambia mume wake kwamba anataka talaka na hakutaka kuishi naye zaidi ya hapo.”

Mwanaume ambaye alichoshwa na mama mkwe wake, alijiua mwenyewe.

Labda inafaa kutaja mambo mawili hapa: Ni dhahiri kwamba mama mkwe si tu ni adui kwa mkwilima wake, lakini ni kawaida yeye kumpenda mkwilima wake kama ilivyo jionesha mwanzoni mwa ndoa. Zaidi yake ni kwamba mama mkwe anajikuta yupo karibu na mkwilima wake kwa sababu ya kutaka kuona binti yake anafurahi. Kwa hiyo, mama mkwe anapoingilia maisha ya ndoa ya binti yake, haiwezekani kumaanisha kuwa kitu chochote isipokuwa kiwe na nia njema. Anamaanisha kuwa na huruma lakini wakati mwingine kwa sababu ya ujinga, huchukua hatua zisizo sahihi au hutoa ushawishi wenye madhara. Kwa hiyo, mtu asiwakosoe sana wake wa aina hii.

Uhusiano wa mama na mtoto ni wa asili ya maumbile ambao hauwezi kuvunjwa kwa urahisi, na yeyote anayefanya bidii ili kufanikisha hilo, kwa hakika atashindwa. Juhudi za aina hiyo ni kinyume cha kanuni za maumbile na haziwezi kuhalalishwa kwa vyovyote vile.

Kama vile mtu mwanaume anavyo wapenda wazazi wake, ndivyo ilivyo kwa mwanamke. Kwa hiyo, ni vizuri zaidi kuwa na uhusiano na wazazi wa wanandoa ambao unanufaisha pande zote mbili. Hii inawezekana tu kama mtu anaonesha heshima na wema. Mwanaume anaweza kwa kutumia busara, heshima, utiifu na kadhalika kuwa na uhusiano mzuri na wazazi wa mke wake. Lazima aoneshe mapenzi yake kwa mtoto wao. Asimlaumu mke wake mbele ya wazazi wake. Aombe ushauri na msaada wa kiroho kutoka kwao. Inapotokea wanatoa ushauri au kukosea kitu fulani, mkwilima anatakiwa kuonesha hilo kwa upole na kimantiki kwamba hapo wamekosea. Asiseme nao kwa ukali.

Mwanaume aliyeoa anatakiwa kuona uhusiano mzuri baina yake na wazazi wa mke wake kama wajibu wake na siri ya mafanikio ya ndoa yao. Matokeo yake ni kwamba matatizo mengi ya kifamilia yanazuiwa yasitokee na mengine mengi zaidi hupatiwa ufumbuzi. Kwa ufupi, si kila mara mama mkwe ndiye anayekuwa na hatia lakini wanamume wanatakiwa kuwa na busara ya kutosha na kuwa fanya kuwa na marafiki.

Wapo wanaume wengi ambao hufurahia uhusiano mzuri na mama wakwe zao.

Bwana Munuchehr ameandika: “mama mkwe wangu ni malaika au hata huzidi. Ninampenda zaidi ya ninavyompenda mama yangu mzazi, kwa sababu ni mwema na muelewa. Kila mara hutusaidia kutatua matatizo yetu. Kuwepo kwake ni dhamana na furaha ya familia yangu na ustawi wetu.”

Hata kama mtu anaye mama mkwe ambaye ni jeuri, mjinga na haiwezekani kuelewana naye, asimfanyie ukali. Wanawake wa aina hii wanaweza kufanya maisha ya mtu kuwa magumu, lakini ni vizuri kila mara kutoa majibu kwa upole dhidi ya tabia yao isiyofaa. Hii ni kwa sababu, kwa kuwa mwema kwao, mtu anaweza akapunguza hatari inayoweza kutokea kwenye ndoa yake.

Wakati huo huo, mwanaume anatakiwa kuwa karibu na mke wake na amfanye mke amwamini yeye. Lazima azungumze naye kuhusu matendo mabaya ya mama yake na kuthibitisha kimantiki kwake matokeo yasiyopendeza yanayoweza kusababishwa na tabia ya mama mkwe wake.

Ikiwa mtu anaweza kutengeneza maelewano ya kina na mke wake, basi matatizo mengi ikiwa ni pamoja na lile la mama mkwe wake litatatuliwa.

Kwa hiyo usidharau tabia njema, uwe na busara na uifanyie wema familia ya mke wako ili mpate kufuzu katika ndoa yenu.

Imamu Ali (a.s) alisema; “Kukuza urafiki ni nusu ya busara.”

Imamu Ali (a.s) pia alisema; Kujumuika na watu na kuwafanyia tabia njema humzuia mtu asifanye matendo mabaya na fitina.”

Imamu Ali (a.s) alisema; Jumuikeni na mfanye wema. Jiepusheni na kununa na kufarakana.”