پایگاه اطلاع رسانی آیت الله ابراهیم امینی قدس سره

Haki Za Kinidhamu Za Mume

Haki Za Kinidhamu Za Mume

Ingawaje mume na mke ambao hutengeneza maisha ya pamoja ya familia, hugawana na kushirikiana katika kuendesha mambo ya nyumba yao, wanaweza kuwa na maoni tofauti kuhusu mambo fulani. Mwanaume anaweza kuhisi kwamba ni yeye ndiye anayetakiwa kuwa na uamuzi wa mwisho kuhusu mambo ya familia, bila kupata upinzani kutoka kwa mke wake.

Wakati huo huo mke wake anaweza akakataa kazi yake kama upande uliomtiifu. Ubishi na ugomvi unaweza ukaanza kwa sababu kila upande unajaribu kuanzisha mamlaka juu ya upande mwingine. Suluhu nzuri zaidi ya tatizo kama hili ni kwamba pande zote zinatakiwa kuacha kujionesha kama unao mamlaka makubwa zaidi kuzidi upande mwingine, na kujaribu kupata ufumbuzi wa matatizo yao kwa njia ya mazungumzo na uelewano wa kina. Hii inawezekana tu kufanikiwa kama pande zote zinaacha ukaidi.

Baadhi ya wanamume huwaamuru wake zao kufanya mambo mengi na kama wakikabiliwa na upinzani, wanadhani ni sahihi kuwashika, kuwaadhibu au hata kuwapiga wake zao. Msimamo huu si sahihi kabisa. Mwanaume wa kipindi cha ujahiliya ambaye alipungukiwa ubinadamu, alifanya mazoea ya kuwapiga na kuwaumiza wake zao.

Mtukufu Mtume (s.a.w) alipiga marufuku kuwapiga wanawake, isipokuwa katika hali isiyozuilika ambapo adhabu huwa wajibu.”

Mtume (s.a.w) pia alisema Nina shangazwa na mwanaume anaye mpiga mke wake, ambapo ni yeye mwenyewe, zaidi ya mke wake ambaye anastahili kupigwa. Enyi watu, msiwapige wanawake zenu kwa kutumia fimbo kwa sababu tendo la namna hiyo lina ulipizaji kisasi.”

Kumuonea mwanamke ambaye kwa utashi wake amekubali kuolewa na mwanamume, ambaye anataka kupata faraja na utulivu na yeye, na ambaye anamtarajia mume wake kushirikiana wote katika matatizo, si sahihi. Kwa kweli Mwenyezi Mungu anamdhamini mwanamke kwa mume wake kwa njia ya ndoa na maonevi ya mwanaume kwa mke wake ni kutokuwa mwaminifu kwa dhamana ya Mwenyezi Mungu.

Imam Ali (a.s) alisema; Wanawake wamedhaminiwa kwa wanamume na kwa hiyo, wao si wamiliki wa bahati zao au mabalaa yao. Wao wapo na nyinyi kama dhamana ya Mwenyezi Mungu, kwa hiyo msiwaumize na msifanye maisha yao kuwa magumu.”

Mwanaume ambaye humpiga mke wake, hulazimisha uharibifu kwenye roho hivyo kwamba anaweza akapata mateso yasiyo elezeka na upendo wa familia na uchangamfu unaweza ukatoweka kabisa. Mwanamume mwenye ghadhabu anaweza kudunisha uhusiano mzuri wa ndoa na mke wake na kushushiwa hadhi? Hii kwa kweli ni aibu.

Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w) alisema: “Enyi wanaume! Inawezekanaje yeyote miongoni mwenu ampige mke wake na baadaye amkumbatie?”

Mwanaume, isipokuwa awe na haki ya pekee kwa mke wake, inayofanana na zile ambazo zitatajwa kwenye sura hii haruhusiwi kisheria kumlazimisha mke wake kufanya jambo lolote au kukimbilia matumizi ya kipigo kuhusu utovu wa utiifu. Mathalani mwanamke kisheria hawajibiki kufanya kazi za nyumbani kama kufagia, kupika, kufua, kutunza watoto, kushona na kadhalika. Licha ya kuwa wanawake walio wengi hufanya kazi hizi za mama wa nyumbani kwa kutaka wao wala si za lazima.

Wanaume wanatakiwa kuwashukuru wake zao kwa kazi zao za ndani ya nyumba. Kwa hiyo, hapana mwanamume mwenye haki ya kuhoji au kumwadhibu mke wake anapokabiliwa na kukataa kwake kutekeleza kazi za nyumbani.

Uislamu unapendekeza adhabu ya kipigo kwenye mifano miwili tu ambapo hali zake hukiukwa:

Mfano wa kwanza; Mwanaume ameruhusiwa kisheria katika Uislamu kupata na kutoshelezwa na tendo la Ndoa na kupata starehe ya kila aina kutokana na uhusiano huu na mke wake. Mke anawajibika kisheria kukubali matamanio ya ngono kutoka kwa mume wake. Kama mwanamke anakataa kumtosheleza mume wake, mume katika hatua ya kwanza anatakiwa amshawishi katika njia na mpangilio unaostahili. Hata hivyo, kama mwanaume anahisi kwamba mke wake anataka kuleta hali hiyo, basi kwa kuchunguza hatua zilizo bainishwa anaweza kumwadhibu.

Mwenyezi Mungu anasema:


الرِّجَالُ قَوَّامُونَ عَلَى النِّسَاءِ بِمَا فَضَّلَ اللَّهُ بَعْضَهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ وَبِمَا أَنْفَقُوا مِنْ أَمْوَالِهِمْ ۚ فَالصَّالِحَاتُ قَانِتَاتٌ حَافِظَاتٌ لِلْغَیْبِ بِمَا حَفِظَ اللَّهُ

 

“Wanaume ni wasimamizi wa wanawake kwa kufadhiliwa na Mwenyezi Mungu baadhi yao juu ya baadhi, na kwa mali yao wanayo yatoa. Basi wanawake wema ni wale wenye kutii na wanao jitihada hata katika siri kwa kuwa Mwenyezi Mungu ameamrisha wajilinde.”
(Quran 4:34).

Kwa hiyo, Qura’ni inamruhusu mume kumpiga mke wake kama hatua ya mwisho ya kutoa adhabu, kama inatokea mke anaonesha tabia mbaya kwa mume wake kuhusu matakwa yake ya ngono.

Hatua ya kwanza ni kutoa ushauri. hatua ya pili; Mwanaume aache kulala kitanda kimoja na mkewe au amgeuzie mgongo na kwa njia hii anatakiwa kuonesha hasira yake. Kama hakuna jibu linalotarajiwa hadi mwishoni mwa hatua ya pili na bado mwanamke anaendelea kukataa, mume anaruhusiwa kumpiga mke wake kidogo.

Mume, hata hivyo, haruhusiwi kuvuka mpaka uliowekwa na kukimbilia kumuonea. Wanaume wanakumbushwa kuhusu yafuatayo: Lengo la adhabu ya kipigo kwa mke wa mtu linatakiwa kuwa njia ya kumuelimisha na si kulipiza kisasi.

Kipigo kinatakiwa kufanywa kwa kutumia mkono au mti mwembamba na mwepezi.

Kipigo kikali cha kuweza kubadilisha rangi ya ngozi kuwa buluu au nyekundu hakiruhusiwi na mhusika lazima apigwe faini (dia).

Kupiga sehemu nyororo na nyeti za mwili kama vile macho, kichwa tumbo na kadhalika, hakiruhusiwi.

Adhabu ya kipigo haitakiwi kuwa kubwa mno hivyo kwamba haitasaidia kuanzisha hasira na fikra mbaya miongoni mwa wanandoa kumwelekeza mke kwenda kwenye kiasi cha kutotii zaidi.

Mwanaume (anaye nuia kumwadhibu mke wake kwa kutumia njia hii) anatakiwa kukumbuka kwamba ataendelea kuishi na mke wake na kwamba upendo wa familia usiharibiwe.

Mwanaume haruhusiwi kumpiga mke wake kama zipo sababu halali zilizomfanya asikubali matakwa yake.

Mathalani kama mke yupo kwenye siku zake za hedhi, saumu ya mwezi wa Ramadhani, awe amevaa vazi la Hija (Ihram) au mgonjwa. Sababu hizi zinakubalika na mwanamume hawezi kumwadhibu mke wake kwa kukataa matamanio yake kwa sababu hizo zilizotajwa.

Mfano wa pili; Mwanamke anaweza kutoka nje hapo tu ambapo ameruhusiwa na mume wake. Akitoka nje bila ruhusa hairuhusiwi kisheria na kufanya hivyo ni dhambi.

Hadith imesimuliwa kwamba Mtume (s.a.w.w) hakumruhusu mwanamke yeyote kutoka nje ya nyumba yake bila ruhusa ya mume wake. Alisema; Mwanamke yeyote ambaye hutoka nje ya nyumba yake bila ruhusa ya mume wake, atapata laana kutoka kwa malaika wote walioko mbinguni na wote wale wanao muona, wawe majini au wanadamu, hadi anaporudi nyumbani kwake.”

Hii ni hali ya mume yeyote ambayo lazima iangaliwe na wake zao.

Lakini wanaume hawatakiwi kuwa wakali sana kwa wake zao. Ni bora zaidi wao kuwaruhusu wake zao kutoka nje kila inapowezekana.

Hali hii ya wanaume haimaanishi kuonesha nguvu au kujaribu kuwashinikiza wake zao, lakini ni njia ya kuwazuia wanawake wasiende kwenye sehemu zisizo pendeza na zisizofaa.

Kuwa mkali sana si tu kwamba ni jinsi isiyofaa, lakini inaweza kuathiri uhusiano wa familia au hata kumsukuma mwanamke kuelekea kwenye utovu wa nidhamu na uovu.

Mwanaume lazima amzuie mke wake asiende kwenye sehemu za mikusanyiko zenye uovu na zisizofaa. Huu ni wajibu wa kidini kwa wanawake kuwatii waume zao. Mwanamke asiye mtiifu anaweza kuadhibiwa na mume wake. Hapa tena adhabu inatakiwa kutekelezwa hatua kwa hatua.

Hata hivyo, mwanamke anaweza kutoka nje ya nyumba yake kwa sababu maalum bila ya ruhusa ya mume wake na wanamume hawaruhusiwi kuwaumiza wake zao katika mifano kama hiyo: Kutoka nje kwa ajili ya kujifunza amri muhimu za dini.

Kutoka nje kwa ajili ya Hija pale ambapo anao uwezo muhimu wa kifedha na kutekeleza Hija.

Kutoka nje ya nyumba kwa ajili ya kulipa deni almuradi deni hilo haliwezi kulipwa bila kutoka nje.