پایگاه اطلاع رسانی آیت الله ابراهیم امینی قدس سره

Elimu Na Mafundisho

Elimu Na Mafundisho

Mwanamke kijana ambaye ndio kwanza kaolewa anao wajibu wa kuendesha mambo ya mume wake na katika hali hiyo atahitaji ujuzi wa kupika, usafi, kunyosha nguo, kushona, kupanga fenicha, kukaribisha wageni wake, kushirikiana na watu wengine, kumtunza mtoto wake na kadhalika.

Mume wake atatarajia mke wake kujua yote haya. Hata hivyo, mategemeo yake yanaweza yasifanikiwe takriban muda wote kwa sababu ujuzi wa mke wake kijana kuhusu utunzaji wa nyumba ama haupo kabisa au upo kidogo sana.

Mtu afanyeje? Hili ni tatizo katika jamii zetu. Wazazi hawajali, wala mfumo wa elimu hauna mipango ya kutosha kukidhi haja hii. Hata hivyo, mtu anatakiwa kupata ufumbuzi wa tatizo hili.

Kwa vile mwanaume anakusudia kuishi na mke wake kwa maisha yake yote lazima amsaidie kumuelimisha, kwa sababu kwa kawaida wanaume huwa na umri mkubwa kuzidi wa wake zao na hivyo wanao uzoefu zaidi.

Mwanaume kwa uvumilivu anaweza kumuelemisha mke wake na kumfundisha vitu ambavyo anavijua. Anweza hata kumuuliza mama yake, dada au shangazi zake kuhusu mambo ambayo hayajui, au anaweza hata kununua vitabu vinavyohusu masomo kama ya kupika, ushonsji, utunzaji wa nyumba na kadhalika.

Mwanaume vile vile lazima amhimize mke wake kusoma vitabu ambavyo vitaonesha kimaadili kuwa ni vyenye manufaa. Lazima asahihishe upungfu wake wa maadili kwa adabu nzuri na sio kwa upinzani, au vinginevyo atageuka dhidi yake.

Mwanaume, kwa kutumia uvumilivu wake, anaweza kumwelimisha mke wake kwa mujibu wa njia yake ya maisha katika kipindi cha miaka miwili ya mwanzo wa ndoa yao. Inawezekana asifaulu asili mia kwa mia lakini bila shaka atakaribia kutosheleza mahitaji.

Elimu ya aina hii inahitaji uvumilivu, muda na busara, lakini mwanaume lazima ajaribu kuipata. Hii ni kwa sababu mwenza mzuri ni mama mzuri kwa watoto wake ni neema kwa mwanaume.

Mojawapo ya mambo muhimu ambayo mwanaume Mwislam aliyeoa anatakiwa kukumbuka ni ukweli kwamba mke wake pia ni Mwislam, na inawezekana awe hatambui utaratibu wa maisha ya Kiislamu na sheria zake. Inawezekana asijue hata kuhusu wudhu, kusali na kadhalika.

Kwa kweli ni wajibu wa wazazi kuwafundisha watoto wao mambo yote muhimu ya Kislamu na maadili. Kwa bahati mbaya, hata hivyo, wazazi hawajui kabisa kuhusu ukweli huu, na bila kuwafundisha mabinti wao kitu chochote kuhusu Uislamu, wanawaozesha. Hivyo wajibu wao huangukia kwenye mabega ya waume wanaowaoa.

Bwana mpendwa! Ni wajibu wako kumzoeza mke wako maadili ya Kiislamu na kumfundisha mambo yaliyohalalishwa na yale yaliyo haramishwa katika dini. Mfanye ajifunze kuhusu tabia za Kiislam. Kama huwezi kufanya hivi, basi tafuta msaada kutoka kwa wengine au fanya mpango wa vitabu na makala zenye elimu ya Uislamu na mwambie asome na kufanya kwa vitendo. Unaweza hata kufanya mpango wa elimu na maelekezo yake kupitia kwa mtu mwaminifu na aliyeelimika.

Kwa ufupi, ni wajibu wa mwanaume kumtia moyo mke wake kumuamrisha kufanya mema na kumkataza kufanya mabaya. Kama mwanamume atafuata wajibu wake huu, basi atafurahia kuwa na mwenza mwenye tabia njema, mwema, muaduilifu na mke mwenye busara.

Hata hivyo, kama mwanamume anaamua kutojali wajibu wake atateseka kwa kuwa na mke mjinga ambaye imani yake ni dhaifu na ambaye hana kinga dhidi ya uovu. Pia mume ataulizwa na Mwenyezi Mungu huko akhera kuhusu uzembe wake huu.

Mwenyezi Mungu anasema kwenye Qurani Tukufu:


یَا أَیُّهَا الَّذِینَ آمَنُوا قُوا أَنْفُسَکُمْ وَأَهْلِیکُمْ نَارًا وَقُودُهَا النَّاسُ وَالْحِجَارَةُ

“Enyi mlioamini jiokoeni nafsi zenu na watu wenu (wa nyumbani – wake zenu watoto wenu nk.,) kutokana na moto ambao kuni zake ni watu na mawe…” (Quran 66:6)

Imamu Sadiq (a.s) alisema: “Aya hiyo hapo juu ilipoteremshwa mmoja wapo wa Waislamu alikuwa analia na kusema; ‘Mimi siwezi kujinusuru hata mimi mwenyewe kutoka kwenye moto wa Jahanamu na ninatakiwa kuwajibika kuinusuru pia familia yangu kutoka kwenye Jahanamu!’ Mtume (s.a.w.) alimwambia mtu huyu: “Ingetosha kama tu ungewaagiza kufanya mambo hayo ambayo wewe unayafanya na uwakataze wasifanye yale ambayo wewe mwenyewe unajizuia kuyafanya.”

Mtukufu Mtume (s.a.w.w) alisema: “Wanaume wameumbwa kuwa viongozi na kuwajibika kwa familia zao, na kwa namna hiyo wanawajibu kwa watu wanaowategemea.”

Mtukufu Mtume (s.a.w.) pia amewakumbusha wanawake: “Waambieni waume zenu wafanye matendo mema kabla hawajawashawishi nyinyi kufanya mabaya.”